Nenda kwa yaliyomo

Mwanzo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Karibu kwenye Wikipedia,
Hadi leo tuna makala takriban 102,872 kwa Kiswahili

Je unapenda kuona Wikipedia yetu kama kitabu? Bofya hapa!
     

     

Kamusi Elezo ya Kiswahili

Karibu kwenye Wikipedia ya Kiswahili!

Wikipedia ni mradi wa kuandika kamusi elezo kamili na sahihi ya maandishi huru.

Kila mtu anaweza kuhariri makala yoyote, kutoa makosa ya lugha, kutohoa maneno na kuendeleza na kukuza makala, kwa kuandika kwa ufupi au kwa urefu. Tunakushauri ujiandikishe na kufungua akaunti. Angalia Wikipedia:Mwongozo ili ujifunze unavyoweza kuhariri au kusanifisha ukurasa. Usisite kushiriki; kwa sababu huu ni mradi wa ushirikiano, na hautaisha kamwe. Kamusi elezo itaimarika vizuri zaidi kila wakati. Angalia ukurasa wa jumuia, ukurasa wa jamii, na ule wa makala za msingi za kamusi elezo ili kung'amua unaweza kufanya kazi zipi ili kuboresha Wikipedia.


Je, wajua...

Kutoka kwenye mkusanyiko wa makala za Wikipedia:

Ngorongoro

  • ... kwamba Hifadhi ya Ngorongoro imepokewa katika orodha ya urithi wa dunia ya UNESCO?
  • ... kwamba Asha-Rose Mtengeti Migiro ni mwanasiasa wa kwanza kutoka nchini Tanzania aliyepata kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa?
  • ... kwamba eneo la Afrika ya Mashariki ndilo ambalo lina uchumi unaokua kwa kasi zaidi katika bara la Afrika!
  • ... kwamba Samia Hassan Suluhu ni rais wa kwanza mwanamke Afrika ya Mashariki? Aliapishwa kuwa rais mara baada ya kifo cha mtangulizi wake, John Pombe Magufuli.


  • Makala ya wiki

    Kimondo cha chuma kilichopatikaka huko Tuva, Urusi

    Vimondo (pia: meteori au meteoridi) ni magimba madogo ya angani yanayozunguka jua. Yanaweza kuangukia duniani yakionekana kama moto angani. Ukubwa wa kimondo ni kuanzia punje ya mchanga hadi kufikia kipenyo cha mita kadhaa. Hivyo kimondo ni kidogo kuliko asteoridi na kikubwa kushinda vumbi la angani. Obiti ya kimondo inaweza kuingiliana na obiti ya dunia au sayari nyingine. Kimondo kikilikaribia gimba la angani kubwa zaidi kinavutwa nalo. Kikikaribia mno dunia yetu kinaingia katika angahewa na kuanguka chini kwa kasi kubwa sana. Njiani kinapashwa moto kutokana na shindikizo la hewa dhidi yake. Kiasi cha joto kinatosha kuchoma kabisa kimondo kidogo hewani. Hii inaonekana kwa macho matupu kama mstari wa moto angani. Kama kimondo ni kikubwa zaidi ni sehemu zake za nje tu zinazochomwa na kiini kinagonga uso wa dunia. Kati ya vimondo kumi vikubwa kabisa duniani ambavyo mabaki yake yanaonekana, kimojawapo ni Kimondo cha Mbozi nchini Tanzania. ►Soma zaidi


    Picha nzuri ya wiki

    Ziara ya Mwalimu Nyerere wa Tanzania mnamo Machi 12, 1985; Rais Nyerere akisikiliza maswali.

    Julius Nyerere (Butiama, 13 Aprili 1922 - London, 14 Oktoba 1999) alikuwa Rais wa kwanza wa Tanzania na Baba wa Taifa. Aliongoza Tanganyika tangu uhuru mwaka 1961 kama Waziri Mkuu, kisha baada ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar mwaka 1964, aliongoza Tanzania kama Rais hadi 1985. Aliunda sera ya Ujamaa na Kujitegemea ambayo iliweka msisitizo kwenye usawa wa kijamii, elimu kwa wote na umoja wa kitaifa. Baada ya kustaafu urais, aliendelea kuishi kwa kuendeleza shughuli za kijamii na kilimo, na alifariki dunia kutokana na saratani ya damu tarehe 14 Oktoba 1999 akiwa London, na kuzikwa Butiama. Je ungependa kusoma zaidi kuhusu Mtu huyu? au ungependa kuchangia zaidi kuhusu mtu huyu? fungua Hapa

    Takwimu ya Wikipedia ya Kiswahili

    • Idadi ya makala: 102,872
    • Idadi ya kurasa zote: 207,112 (pamoja na kurasa za watumiaji, majadiliano, msaada n.k.)
    • Idadi ya hariri: 1,468,102
    • Idadi ya watumiaji waliojiandikisha: 84,112
    • Idadi ya wakabidhi: 14
    • Idadi ya watumiaji hai: 381 (Watumiaji waliojiandikisha na kuchangia katika muda wa siku 30 zilizopita)
    Bofya hapa kwa kupata namba za sasa
    Katika mwezi wa Agosti 2025 wikipedia ya Kiswahili iliangaliwa mara milioni 7.79 hivi, ambayo ni sawa na mara 251,607 kwa siku au mara 10,483 kila saa ambalo ni ongezeko la mara 4.5 ukilinganisha na mwaka 2024 mwezi wa Agosti. Asilimia 52 za wasomaji wetu wako Tanzania, asilimia 13 wako Kenya, asilimia 18 wako Marekani na mnamo asilimia 10 wako Ulaya.
    Angalia idadi ya wasomaji kwa makala mbalimbali
    (fungua anwani kwa browser yako, ondoa majina yaliyopo na ingiza jina la makala (hadi makala 10) unayopenda. Unaweza kubadilisha kipindi cha taarifa utakachoona; takwimu kabla ya 2015 hapa)
    • na makala 100 zilizotazamiwa zaidi "Topviews" kwa kipindi fulani.
    (unachagua kati ya makala 100 kwa mwezi au kwa siku)

    Michango ya wanawiki: angalia hapa michango ya mtumiaji kwenye kila mradi wa Wikimedia (andika jina la mtumiaji kwenye sanduku)

    Jumuia za Wikimedia

    Commons
    Ghala ya Nyaraka za Picha na Sauti
    Meta-Wiki
    Uratibu wa Miradi yote ya Wikimedia
    Wikamusi
    Kamusi na Tesauri
    Wikitabu
    Vitabu vya bure na Miongozo ya Kufundishia
    Wikidondoo
    Mkusanyiko wa Nukuu Huria
    Wikichanzo (Wikisource)
    Matini za vyanzo asilia kwa Kiswahili
    Wikispishi
    Kamusi ya Spishi
    Wikichuo
    Jumuia ya elimu
    Wikihabari
    Habari Huru na Bure

    Wikipedia kwa lugha nyingine

    Wikipedia kwa lugha nyingine